> Hizi ndizo siri za kujenga penzi imara | MAPENZI

Hizi ndizo siri za kujenga penzi imara

 Kuelezea Hisia
Moja kati ya msingi wa kuwa na mahusiano imara ni uwezo wa kuonesha hisia zako kwa parter wako na kujua kumsikiliza.kusema “nimekuelewa” haimaanishi “nimekubaliana na wewe” hivyo ni vema kumsikiliza mwenzio kuliko kukubali kila kitu ilimradi kuwe na amani.

 Panga Quality time na partner wako

Hasa uhusiano unapozidi kukua ni muhimu kuwa na muda wa pekee ambao mtazungumza kuhusu uhusiano wenu pekee na mipango muhimu ya baadae.

Bishaneni lakini kwa jambo maalumu
ule mpango wa kukusanya malalamiko kibao ya mwezi wako mfano pale mnapogombana kuhusu kuchelewa on a date then mnaanza kuongezea na vitu vingine kibao kama kutompigia simu , kutovaa vizuri , kutokujali na mengine kibao.Kubishana kuhusu mambo mia kwa wakati mmoja ni vigumu kukabiliana nako hivyo bishaneni mara moja jambo linapotokea.

 Ongeza vitu vipya katika mahusiana

Ile safari ya kwenda wote kwa mara ya kwanza zanzibar au kujifunza kozi mpya basi ni vyema kuvifnya vitu hivi vipya pamoja. Ni vyema kukua pamoja , na kupeana changamoto pamoja mkiwa na uzoefu mpya mlioupata pamoja.

 Onesha Shukrani

kila mtu hapendi kuonekana yupo chini lakini kumshukuru mwenzako kwa safari aliokupeleka mbuga za wanyama au pesa za matumizi alizokupa kutamfanya asione kwamba unamchukulia poa na kutamfanya aendelee kukudhamini na kukuzidishia mambo mazuri.

 Omba ruhusa kuongelea jambo fulani

Simaanishi uombe kwa unyonge bali pale unapotaka kuzungumza na mwezako kuhusu jambo lilalogusa sana maisha yenu ni vizuri kuuliza kwanza kama ni wakati sahihi.


 Msisahau Mlianzaje
kumbukeni mlivyoanza , jinsi mapenzi yalivokua , hata kama mmeishi kwa miaka mitano pamoja msiache zile hisia za mwanzo zikaondoka. Fanya juhudi za kuwa mbunifu na mshangaze mwezio.

 kukua
kukua na kubadilika kama wewe kutafanya mahusiano yenu kuwa bora zaidi. Moja ya vitu muhimu kabisa katika mahusiano ni kujifunza kuhusiano na wewe mwenyewe zaidi au sawa na utakavyojifunza kuhusu partner wako. Kwa kuangalia vitu unavyofanya ukiwa na partner wako na jinsi anavyokuletea changamoto itakufanya na wewe ukue kilazima.

 Usiwaache Rafiki zako

Ni dhahiri kwamba unataka mchumba wako ndio awe wa kwanza kupata habari nzuri pale inapotokea au mtu wa kwanza kufuta machozi yako pale unapopata shida lakini mara nyingine utamuhitaji rafiki yako hasa kwa wanawake kuna vitu ukimwambie mchumba wako hawezi kukuelewa lakini ukijadiliana na rafiki yako wa kike anaweza kukusaidia na kukupa ushauri.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright MAPENZI Published.. .
Back To Top