> Je unajua ni mambo gani muhimu ambayo mwanamke anapenda kutendewa na mpenzi wake..Ingia hapa kuelimika zaidi | MAPENZI

Je unajua ni mambo gani muhimu ambayo mwanamke anapenda kutendewa na mpenzi wake..Ingia hapa kuelimika zaidi

ELIMU ya mapenzi ni jambo pana sana huwezi kujifunza ukamaliza ila hapa tunakumbushana tu vile vitu muhimu muhimu ambavyo unapaswa kuwa unavikumbuka ili kudumisha penzi lako na kulifanya lenye furaha kila wakati na vilevile wanaume wa siku hizi wamekuwa wavivu sijui au ni hawafahamu vitu muhimu ambavyo mwanamke anapaswa kuvipata kutoka kwao..Basi kwakulitambua hilo nimewaletea mada hii nzuri kabisa hususani kwa wanaume ili ujifunze kumfurahisha mpenzi wao kila wakati..

Kushindwa kuwa na elimu hii, wanaume wengi wamejikuta wakitumia ukali kuwatawala wake zao, jambo ambalo limekuwa likizidisha migogoro ya kimapenzi na hatimaye wapenzi huachana. Yafuatayo ni mambo muhimu ambayo wanawake hupenda watendewe na wapenzi wao.

KUTATULIWA MATATIZO
Wanawake wengi hutegemea kuwa wanapokuwa na wapenzi watasaidiwa katika matatizo ya kimaisha na migogoro ya kimawazo. Kwa mfano ushauri juu ya maisha yao, kulindwa na hatari za kimaisha, kusaidiwa katika shida na kuongozwa pale wanapohisi kushindwa kufanya jambo. Kama mwanaume hatamfanyia mpenzi wake hili atakuwa amekosa sifa za kuteka penzi la mwanamke.

KUBEMBELEZWA
Wanawake hupenda kubembelezwa pale wanapokuwa na huzuni, wengi wao hawapendi kukaripiwa, mara nyingi hupenda kuungwa mkono wanapokuwa na misuguano na wengine. Ili mwanaume amteke kimapenzi mwanamke lazima awe nyuma yake hata kama atakuwa na kosa. Wanawake wengi hupenda kuelimishwa zaidi kuliko kufokewa.

KUWA NAMBA MOJA 
Safari ya penzi la mwanamke haishii kwenye kumpata na kumliki, kisha kujisahau kwa kisingizio kuwa umemuoa au umemvisha pete ya uchumba, ni zaidi ya hapo. Jambo la tatu ambalo wanawake wengi huhitaji ni kuwa namba moja au kupendwa.
Wanapenda watangulizwe katika mapenzi na kusiwepo na mwingine wa kuchukua nafasi yao katika mazungumzo na mapenzi kwa ujumla. Wanawake hawapendi kuitwa majina mabaya kwa mfano mjinga, Malaya au kulinganishwa na wanawake wenzao wabaya.

KURIDHISHWA KWENYE TENDO
Hata kama utakuwa na kiwango kikubwa cha mapenzi juu ya mpenzi wako kwa kiwango gani, ukiwa dhaifu katika tendo la ndoa utayumbisha penzi lako. Ni wajibu wa mwanaume kuhakikisha kuwa anamtosheleza mpenzi wake katika tendo hilo. Utundu unahitajika ili kumkata kiu mpenzi wako.

MAZUNGUMZO
Wanawake wanatajwa kuzungumza maneno 25,000 kwa siku, huku wanaume wakibaki na kiwango cha maneno 5,000 kwa siku, hii ikiwa na maana kuwa wanawake hupenda zaidi kujieleza walivyo mbele ya wengine. Kwa msingi huo wakizuiwa wasiongee hujiona kama wanakosa nafasi muhimu ya kueleza mawazo yao. Kama una mpenzi wako mpe uhuru wa kuzungumza na kumsikiliza

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright MAPENZI Published.. .
Back To Top