> MALAVIDAVI..Msichana hapendezwi na maneno haya awapo kitandani na mpenzi wake | MAPENZI

MALAVIDAVI..Msichana hapendezwi na maneno haya awapo kitandani na mpenzi wake



1. Mvulana wako wa kwanza na mimi nani bora?. Kwanza ni ujinga ulioje kujifananisha na mtu ambaye aliwahi kupita kwa msichana wako. Huna haja ya kutaka kujilinganisha naye wewe mpe ujuzi ujuao ili akuone wewe bora akusifie mwenyewe 


2. Kulitaja jina la msichana mwingine iwe kwa kunsifia au kumzungumzia kwa vyovyote vile. Anajua kuwa wewe una urafiki na wasichana wengi lakini tabia ya msichana hupenda kufikiriwa yeye peke yake tu na s mwingine hivyo ukimtaja taja huyo msichana mwingine inaonesha kuwa huyo msichana mwingine ndio yupo akilini mwako

3. Umenipa burudani usithubutu kumwambia hivi mara baada ya kumaliza kwa sababu wengine hufikiria vibaya na kujiona kama umemchukulia yeye ni malaya na ndio maana umelichukulia tendo kama hilo ni burudani na si tendo la kihisia

4. Mpenzi wangu wa zamani alikuwa anapenda kunifanyia hivi au mimi nimfanyie hivi. Huo ni ujinga wa wajinga wachache ambao wanashindwa kufikiria. Hivi ni nani ambaye anapenda kusikia mwingine akisifiwa? Basi kama wewe hupendi kwanini umsifie mpenzi wako aliyepita? Mbele ya msichana wako unadhani atajisikiaje? Sio vizuri

5. Tufanye haraka kuna sehemu naenda baada ya dakika kadhaa. Kama ulikuwa na haraka ni heri ungetafuta muda mzuri muafaka na si kumuharakisha mwenzio. Wasichana hupensa kuutumia muda huu vizuri kwa kuandaana na kufanya starehe taratibu sasa ukiwa na haraka na yeye hajafika anapopataka? Itakuwaje? Acheni haraka zisizo na msingi wowote

6. "wewe unajua sana kila siku kama msichana wangu fulani" yale yale. Kila msichana anataka sifa zake peke yake anapenda kujijua yeye ni bora kuliko yeyote akiwa kitandani. Sentensi kama hii inaharibu akili yake na kumfanya ajfikirie mara mbili na kujiuliza "unamfikiria yeye wakati unafanya mapenzi na mimi? Unatamani ungekuwa na yeye wakati huu?" hivyo ndivyo anajiwazia ukishasema hayo. Umeipenda?

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright MAPENZI Published.. .
Back To Top