> Mambo yanayosababisha mwanamke kumsaliti mpenzi wake.... | MAPENZI

Mambo yanayosababisha mwanamke kumsaliti mpenzi wake....



Usaliti ni kitu kibaya sana. Ni matokeo ya ukosefu wa ubinadamu. Ni kwenda nje ya makubaliano ya kimsingi. Ni uamuzi wa mtu kushusha thamani yake mwenyewe. Ni kujidhalilisha kwa makusudi. Ni kujionesha mbele ya umma kwamba wewe hufai, huaminiki.

Aya hiyo, ikupe mantiki kuwa msaliti siyo binadamu. Sasa basi, endapo utaamua kufanya hivyo, ujijue kwamba unajidhalilisha na unajipa sifa mbaya mbele ya jamii. Kwamba unajipeleka kwenye ukurasa ambao kila atakayekusoma, atakutafsiri kuwa hufai, kwani huna maana.

Kwa nini watu wanasaliti? Hapa nieleze kuwa usaliti ambao naujengea hoja siyo ule wa kuchukua maneno upande mmoja na kupeleka sehemu nyingine, la hasha! Namaanisha vitendo vya kumchepuka mwenzi wako. Yaani unakwenda kufanya mapenzi nje ya ndoa au kuhusika na mtu tofauti na mchumba au mpenzi wako anayekubalika.

Usaliti unasababishwa na vitu vingi lakini kikubwa ni tamaa. Inawezekana ikasababishwa na hulka ya kutaka kuwa na wengi au kuvutwa na fahari ya macho. Umemuona, akakuvutia kisha ukataka uone ndani pakoje. Huu ni ulemavu mkubwa sana unaotawala vichwa vya wengi.

Fedha ni janga kuu. Wanawake kwa wanaume wanaendeshwa na pesa, hivyo imekuwa ikiamua hatma ya uhusiano wa watu wengi. Nilishawahi kuandika kuwa “fedha ni dereva wa moyo”, kwamba mapenzi kwa sehemu kubwa yanaamuliwa na fedha. Kama huna kitu, utasalitiwa tu!

Tuachane na kipengele cha fedha na tamaa, kwa upande wa wanawake, zipo sababu mbalimbali ambazo huwafanya wachepuke ama nje ya ndoa au ‘kuchutama’ kwa mwanaume wa pembeni tofauti na boyfriend/mchumba wake. Sababu zao zipo kisaikolojia zaidi.

Ni muhimu kwa kila mtu kutambua haya kwa sababu kuu mbili; Mwanaume kujua namna ya kuishi vizuri na mwenzi wake ili ajue nyakati za hatari za kusalitiwa. Pili, mwanamke kujichunga, kuvaa uimara wakati wowote na kuepuka ushawishi wa kusaliti. Kuna ushauri muhimu sana ndani ya makala haya.

Pamoja na sababu nitakazozieleza ambazo nyingine zinaonesha kuwapendelea wanawake kwamba wakati mwingine husaliti kutokana na tabia za wenzi wao, ila ukweli ubaki kwenye kipimo chake kuwa msaliti yeyote anakuwa amejiondoa kwenye taswira halisi ya ubinadamu na kujifananisha na mnayama.

Kitendo cha kuvua nguo mbele ya mwanaume huyu, kesho eti kwa sababu umekosewa ndiyo ukafanya hivyohivyo kwa mwingine, ni sawa na kujifananisha na wanyama. Pointi hapa ni kuwa unajifananisha na wanyama kwa sababu wao huwa hawavai nguo. Ni kama wewe tu unayevuavua ovyo na kuruhusu wanaume tofautitofauti wakuone.

Wanyama huwa hawafanyi makubaliano ya kueleweka, isipokuwa hupandana kiholelaholela. Nawe kwa sababu maisha yako hayapo kwenye mtiririko unaokubalika, unaamua kufanya kama wanyama. Leo unatumika kwa huyu, keshokutwa upo na mwingine. Inawezekana unafurahia maisha hayo lakini siyo sawa kabisa. Hizo ulizonazo ni hulka za wanyama.

Kuhusu sababu ambazo huwafanya wanawake kuamua kuziendea kinyume ndoa au uhusiano wao wa kimapenzi na kufanya usaliti, soma sababu 10 zinazofuata. Ukisoma kinagaubaga, utaelewa wapi pa kushika na nini cha kufanya. Ni mapenzi tu na mapito yake.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright MAPENZI Published.. .
Back To Top